welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Thursday, 23 October 2014

HABARI HII YA KUSIKITISHA HAUSIGELI ALIVYOMFANYIA MTOTO

Mtoto, Samwel John akiwa na maumivu makali aliyoyapata baada ya kujeruhiwa kwa kisu. Akizungumzia mkasa huo kwa masikitiko makubwa uliojiri hivi karibuni maeneo hayo, baba mzazi wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la John alisema kuwa, siku ya tukio hilo alimuona hausigeli huyo akiwa amemshika mkono mwanaye huku akiwa na majeraha kwenye jicho na kichwani. Alisema alipomuuliza nini kimetokea, hausigeli huyo alimjibu kuwa mtoto Samwel aligongwa na pikipiki.

Unyama! Dada wa kazi (hausigeli), aliyetajwa kwa jina moja la Rachel, mkazi wa Tabata-Shule jijini Dar, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuchukua kisu jikoni kisha kumchomachoma nacho mtoto, Samwel John (4) anayeishi nyumba ya jirani. 

John alisema kwamba, hausigeli huyo alimwambia kuwa mtoto alikuwa amegongwa na pikipiki lakini mtoto alikataa huku akimnyooshea kidole yule dada wa kazi.

No comments: