welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Thursday 4 December 2014

HUYU ZARI NI NANI?!MFAHAMU KWA KINA HAPA..PIA KAMA ULIMISS DIAMOND KUWA MGENI RASAMI

“Habari mpya ni kwamba Diamond Platnumz atakuwa mgeni rasmi katika pati ya Zari All White Ciroc, najihisi niko sahihi kwa sababu sioni kama kuna ushindani wowote, huyu ni mtu wangu na itabaki kuwa hivyo,” 
Licha ya kumzidi miaka 10, Zari atangaza rasmi kuwa ni mtu wake wa karibu kwa sasa. 

Johannesburg/Dar. Baada ya kuukimbia ukweli kwa kipindi cha mwezi mmoja, mwanamuziki Diamond Platnumz amethibitisha kuwa na uhusiano baina yake na staa maarufu kutoka Uganda, Zari ‘The Boss Lady’ na kwamba atakuwa mgeni rasmi katika hafla yake ijulikanayo ‘Zari All White Ciroc’ itakayofanyika mwezihuu. 
Nyota huyo aliyevunja rekodi kwa kunyakua tuzo tatu za Channel O Music Video Awards (ChoMVA) wikiendi iliyopita, amekuwa akijadiliwa katika mitandao ya Tanzania na nje ya nchi kwa kuonekana na wanawake tofauti kila wakati, hali inayowachanganya mashabiki wake. 
Hata hivyo, Diamond hajasita kuelezea hisia zake za sasa na kwamba yupo tayari kuhudhuria hafla hiyo, inayotarajiwa kufanyika Desemba 18. 
“Nitakuwapo katika hafla hiyo, ni lazima nimuunge mkono, mbona kuna wengi wanaunga mkono na watu hawasemi, kama wanavyokaa kimya kwa wengine nahuku iwe vivyo hivyo,” alisema Diamond huku akishindwa kukiri moja kwa moja kwamba ana uhusiano na Zari, “waswahili wanasema A na B yote majibu.”
Kwa upande wa Zari ambaye ndiye aliyekuwa msindikizaji mkuu wa Diamond wakati wa utolewaji wa tuzo hizo, alitangaza rasmi kwamba nyota huyo ndiye atakayekuwa mgeni rasmi katika hafla yake. 

“Habari mpya ni kwamba Diamond Platnumz atakuwa mgeni rasmi katika pati ya Zari All White Ciroc, najihisi niko sahihi kwa sababu sioni kama kuna ushindani wowote, huyu ni mtu wangu na itabaki kuwa hivyo,” alisema Zari. 
Zari ni nani?



Jina lake halisi anajulikana kama Zarinah Hassan maarufu Zari. Alizaliwa Septemba 23, 1980 huko Jinja, Uganda, kati ya shule alizosoma ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jinja. Alikwenda Kampala na baadaye jijini London ambako alipata Diploma ya Cosmetology.Zari alianza kujishughulisha na masuala ya muziki akiwa shule ya msingi. Kwa kuungwa mkono na familia yake mwaka 2007, alirekodi wimbo wa kwanza Oliwange (Wewe ni Wangu), albamu hiyo ilimpa tuzo Channel O ikiwa video bora ya Afrika Mashariki. Tangu hapo alitoa vibao kadhaa. 

Mwanamuziki huyo ambaye ana asili ya India, Burundi, Uganda na Somalia, mwaka 2009 alipata tuzo ya mwanamuziki bora wa kike, huku mwaka 2008 akishinda tuzo ya Channel O akiwa mwanamuziki bora Afrika Mashariki. 


Usiyoyajua kuhusu Zari
Zarinah ni mwanamuziki anayeishi Afrika Kusini na mumewe Ivan Semwanga anayedaiwa kuwa ametengana naye kwa sasa. Ana watoto watatu aliozaa na mumewe huyo ambao ni Pinto, Didy na Quincy ambao nao pia wanaishi Afrika Kusini. Ni mjasiriamali na mfanyabishara maarufu na tajiri anayeuza zaidi vipodozi na nguo. Anamiliki magari ya bei ghali.

No comments: