welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Friday 17 October 2014

BWANA WA WASTARA ADAIWA KUMPA MIMBA MHUDUMU

MSANII wa filamu za Kibongo ambaye ni Mtangazaji wa Channel Ten, Bond Bin Sinan, anadaiwa kumpa mimba mhudumu wa baa maarufu ya Break Point (BP) iliyopo Kijitonyama, Dar, anayejulikana kwa jina moja la Grace (pichani). Mhudumu wa baa anayejulikana kwa jina moja la Grace anayedaiwa kupewa mimba na Msanii wa filamu za Kibongo, Bond bin Sinan.Akizungumza na gazeti hili kwa huzuni kubwa, Grace alisema yeye na Bond ambaye kwa sasa anadaiwa ni bwana wa mwigizaji Wastara Juma, walikutana maeneo ya Masaki, Dar, Februari, mwaka huu ambako alikuwa akifanyia kazi awali na kuanzisha uhusiano wa kimapenzi. 


Alisimulia kuwa, katika kipindi hicho walikuwa kwenye mahaba niue ambapo mara nyingi alikuwa akitoka kazini anamfuata nyumbani kwake Mwananyamala, Dar.Aliendelea kufunguka kwamba alipomwambia tu kuwa ana ujauzito wake ndipo mambo yalibadilika huku jamaa akitibuka utadhani kamwagiwa pilipili iliyosagwa. 
Grace akiongea jambo.“Ukweli mwazoni mapenzi yalikuwa shatashata lakini baada ya ujauzito, jamaa aliniruka futi mia.
“Mwanzoni alitaka nikatoe lakini nikakataa na kumwambia kwa nini niue kiumbe kisicho na hatia ndipo akaingia mitini mpaka leo na ujauzito una miezi sita. “Kila nikimwambia anasema siyo wake, ananitukana na mwisho aliniambia kwamba nisubiri mtoto azaliwe ndiyo tukapime DNA (vinasaba), sasa nateseka kuulea ujauzito peke yangu.“Naendelea kulea hii mimba, najua Mungu atanisaidia, nitajifungua salama na mwanangu nitamlea lakini inaniuma sana kutokana na majibu anayonipa na matusi ya kila wakati. 
Manii wa filamu za Kibongo, Bond Bin Sinan akiwa na Wastara.“Nimefikia hatua hii ya kuzungumza ili walau mnisaidie jamani maana naona ananisumbua na hanielewi.“Kuna siku nilikutana na aliyekuwa mpenzi wake (Anti Lulu), nikamwambia kila kitu akaahidi kunisaidia,” alisema Grace akimwaga chozi. 
BOND ANASEMAJE?
Ili kupata mzani wa habari hiyo, gazeti hili lilimsaka Bond na kummwagia kila kitu ambapo alikuwa na haya ya kusema: “Huyo dada mimi simfahamu na ninaona wamepanga kunichafua yeye na Anti Lulu kwa sababu nina meseji nyingi sana za huyo dada, nimewasiliana naye Facebook akisema yupo naye hapo kazini kwake hivyo naomba mpotezee hizo habari siyo za kweli.” 
Gazeti hili lilifanikiwa kuziona meseji za Bond alizokuwa akiwasiliana na Grace katika mtandao wa kijamii wa WhatsApp ambazo zilikuwa zimejaa matusi yasiyoandikika gazetini huku akimtaka mwanadada huyo kusubiri ajifungue ndipo wakapime DNA ili kujua ukweli.

No comments: