MSANII
wa filamu za Kibongo ambaye ni Mtangazaji wa Channel Ten, Bond Bin
Sinan, anadaiwa kumpa mimba mhudumu wa baa maarufu ya Break Point (BP)
iliyopo Kijitonyama, Dar, anayejulikana kwa jina moja la Grace
(pichani). Mhudumu wa baa anayejulikana kwa jina moja la Grace
anayedaiwa kupewa mimba na Msanii wa filamu za Kibongo, Bond bin
Sinan.Akizungumza na gazeti hili kwa huzuni kubwa, Grace alisema yeye na
Bond ambaye kwa sasa anadaiwa ni bwana wa mwigizaji Wastara Juma,
walikutana maeneo ya Masaki, Dar, Februari, mwaka huu ambako alikuwa
akifanyia kazi awali na kuanzisha uhusiano wa kimapenzi.
Alisimulia kuwa, katika kipindi hicho walikuwa kwenye mahaba niue
ambapo mara nyingi alikuwa akitoka kazini anamfuata nyumbani kwake
Mwananyamala, Dar.Aliendelea kufunguka kwamba alipomwambia tu kuwa ana
ujauzito wake ndipo mambo yalibadilika huku jamaa akitibuka utadhani
kamwagiwa pilipili iliyosagwa.
Grace akiongea jambo.“Ukweli mwazoni mapenzi yalikuwa shatashata lakini baada ya ujauzito, jamaa aliniruka futi mia.
“Mwanzoni alitaka nikatoe lakini nikakataa na kumwambia kwa nini niue
kiumbe kisicho na hatia ndipo akaingia mitini mpaka leo na ujauzito
una miezi sita. “Kila nikimwambia anasema siyo wake, ananitukana na
mwisho aliniambia kwamba nisubiri mtoto azaliwe ndiyo tukapime DNA
(vinasaba), sasa nateseka kuulea ujauzito peke yangu.“Naendelea kulea
hii mimba, najua Mungu atanisaidia, nitajifungua salama na mwanangu
nitamlea lakini inaniuma sana kutokana na majibu anayonipa na matusi ya
kila wakati.
Manii
wa filamu za Kibongo, Bond Bin Sinan akiwa na Wastara.“Nimefikia hatua
hii ya kuzungumza ili walau mnisaidie jamani maana naona ananisumbua na
hanielewi.“Kuna siku nilikutana na aliyekuwa mpenzi wake (Anti Lulu),
nikamwambia kila kitu akaahidi kunisaidia,” alisema Grace akimwaga
chozi.
BOND ANASEMAJE?
Ili kupata mzani wa habari hiyo, gazeti hili lilimsaka Bond na
kummwagia kila kitu ambapo alikuwa na haya ya kusema: “Huyo dada mimi
simfahamu na ninaona wamepanga kunichafua yeye na Anti Lulu kwa sababu
nina meseji nyingi sana za huyo dada, nimewasiliana naye Facebook
akisema yupo naye hapo kazini kwake hivyo naomba mpotezee hizo habari
siyo za kweli.”
Gazeti hili lilifanikiwa kuziona meseji za Bond alizokuwa
akiwasiliana na Grace katika mtandao wa kijamii wa WhatsApp ambazo
zilikuwa zimejaa matusi yasiyoandikika gazetini huku akimtaka mwanadada
huyo kusubiri ajifungue ndipo wakapime DNA ili kujua ukweli.
No comments:
Post a Comment