NINAMFAHAMU
Blandina Changula maarufu kama Johari, tokea akiwa underground wa
maigizo katika kikundi cha Kaole, kabla hajapata jina linalomfanya kuwa
mmoja wa wakongwe katika filamu Tanzania.
Wakati
ule akichipukia, alikuwa mmoja kati ya chipukizi waliokuwa wanaonyesha
wazi kwamba watakuja kuwa waigizaji wazuri. Anapatia sehemu nyingi
katika sanaa, lakini utampenda zaidi Johari akiigiza sehemu inayohitaji
majonzi, au mtu anayetaka kuhurumiwa.
Johari
anaweza kutoa machozi wakati wowote akitaka. Anaweza kucheka kwa sauti
na furaha dakika hii, lakini inayofuata akatoa machozi mengi hadi
unashangaa. Napata wasiwasi ninapomuona akitoa machozi katika misiba,
hujiuliza kama analia kweli kwa uchungu au ni mbwembwe tu za maigizo ili
watu wajue ana uchungu! Kama
nilivyosema mwanzo, Johari ni mmoja kati ya waigizaji wasichana
ninaowafahamu zaidi katika fani, pengine kuliko masistaduu wengi
waliopata majina makubwa katika miaka ya hivi karibuni. Anajua kufanya
kazi kwa kweli na ni lazima hawa waliomkuta, wampe heshima anayostahili
kwa sababu anao mchango mkubwa sana katika game.
Ninafahamu
kwamba Vicent Kigosi, wakati huo naye akianza kuogelea kwenye umaarufu
wa filamu, alikuwa akitoka na dada huyu. Mara kadhaa nimewahi kuwakuta
pamoja na kwa maana hiyo, hakuna mdau asiyetambua uhusiano wao.
Ni
kutokana na uhusiano huo, ambao awali ulionekana kama wenye mwelekeo wa
kuzaa ndoa, wawili hao walifungua kampuni yao, RJ, kila herufi
ikiwakilisha mwanzo wa majina yao ya kisanii.
Lakini
kama tunavyofahamu, wawili hawa walianza chokochoko katika uhusiano wao,
baada ya kuwepo kwa taarifa za Ray kuchepuka na Chuchu Hans, binti
mdogo aliyemkuta Johari katika fani. Mwanzo ilikuwa ni siri, lakini
baadaye ikathibitika kuwa ni kweli kiasi kwamba hata Johari akakubali na
kumwaga manyanga.
Sijui,
labda kwa sababu ni wasichana, wawili hawa wamekuwa wakipigana vijembe
kila wanapokaa pamoja au kukutana. Mara moja waliwahi kuripotiwa
kupigana katika ofisi za RJ.
Wiki
iliyopita, wawili hawa waliripotiwa kutukanana kwa mara nyingine na
almanusura wazichape. Walikutana katika eneo ambalo Johari alikuwa
ameweka kambi yake, Chuchu akiwa ameambatana na Ray.
Niseme
wazi kuwa ingawa ni vigumu kuzungumzia hisia za watu kimapenzi, lakini
kwa uzoefu wa wawili hawa, inaonekana kama wanaishi maisha flani
yanayokwenda kinyume na ustaarabu wa kisasa.
Nianze na
Chuchu. Mara zote ugomvi unapotokea, binti huyu huwa amemfuata Ray
katika eneo analojua kabisa kuwa Johari atakuwepo, hivi kwa kutumia tu
busara zake za kawaida, kwa nini huwa hajiepushi kusogelea? Kwa sababu
anajua kuwa yeye alimpora mwenzake mtu wake.
Hivi
anapokwenda ofisini kwa Ray kwa mfano, akijua kabisa Johari pia yupo,
haoni kama anayakaribisha matatizo makusudi? Maana yake ni kuwa
anakwenda pale akitamba kwamba hawezi kufanywa lolote!
Na
Johari, kwa umri ulionao, huoni kama ni kujifedhehesha tu kumpigania
mwanaume unayejua kabisa hana mapenzi nawe? Huhisi watu wanaweza kukuona
ni mshamba wa mapenzi?
No comments:
Post a Comment