welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Wednesday 31 December 2014

WEMA AFUNGA MWAKA KWA KILIO!

Mkali katika tasnia ya filamu Bongo, Wema Sepetu ‘Madam akilia huku akibembelezwa na shost yake Aunt Ezekiel.
OHOOOO! Wakati pazia la mwaka 2014 likifungwa leo, mama la mama, Wema Sepetu ‘Madam’ ameuaga mwaka huo kwa staili ya kilio cha nguvu, mchapo hatua kwa hatua huu hapa... 

Tukio hilo lililozua maswali mengi bila majibu, lilitokea usiku wa kuamkia Desemba 29, mwaka huu kwenye shoo ya Madam ya kuuaga mwaka 2014 (Say Good Bye To 2014) iliyofanyika katika Klabu 71, Tegeta-Kibaoni jijini Dar. 
Kabla ya kukutwa na kisanga hicho kwenye shoo hiyo ambayo Madam aliiandaa chini ya Kampuni yake ya Endless Fame, shoo mbalimbali kutoka wasanii kibao wa Bongo Fleva kama Barnaba, Izo Business, Bob Junior na wengine wengi zilihusika kisha baadaye Wema alipanda jukwaani na kumtambulisha msanii wake mpya ajulikanaye kwa jina la Ally Luna. 
“Ally Luna atasimamiwa shughuli zote za kimuziki na mimi chini ya kampuni yangu Endless Fame, na atapata huduma zote za muhimu kama inavyofanyika kwa msanii wangu wa zamani, Mirrow,” alisikika Wema. 

Mara baada ya shoo hiyo iliyoambatana na bethidei ya mtangazaji wa Clouds FM, Soudy Brown kumalizika, Wema alikutwa na mapaparazi nje ya ukumbi huo akiangua kilio cha nguvu ambacho hakikujulikana moja kwa moja ni cha nini

No comments: