welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Friday 17 October 2014

BAADA YA MISS TZ 2014 KUANDAMWA SANA MITANDAONI, MISS TZ 2012 AMEAMUA KUMSHAURI

Kama na wewe unakerwa au haupendi jinsi ambavyo Miss Tanzania wa 2014 Sitti Mtemvu amekua akiandamwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu umri wake na elimu yake baada ya kushinda taji hilo weekend iliyopita basi uko upande mmoja na Miss Tanzania wa 2013Brigitte Alfred. 
Kupitia page zake za twitter na Instagram Brigitte pamoja na mengine ameandika >>> ‘Mazuri mengi yanawapita lakini inapotokea skendo mnajadili milele ndio maana hatuendelei, natamani tungeweka hizi nguvu za matusi kwenye vitu vya kujenga‘
Baada ya hiyo sentensi Brigitte alimuandikia Sitti kwa kusema >>> ‘Sitti usiwaruhusu watu wakuandame sana, ikizidi warudishie tu taji lao’
Kwenye tweets nyingine za wiki hii baada ya Sitti kutangazwa mshindi Brigitte aliandika ‘mngejua siasa za huko Miss World hata msinge jisumbua kumshambulia huyu msichana kiasi hicho, mtihani wa Miss Tanzania sio tu siku ya fainali ndio maana kunakua na camp ya siku 30′

Kama msomaji….. maoni yako ni yapi kuhusu hii ya Miss Tanzania kuongelewa kila kukicha? naomba niachie comment yako hapa chini mtu wangu
Chanzo:Millardayo

No comments: