welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Monday 8 September 2014

MSANII BONGO MOVIE ATIA KINYAA

Stori: Mayasa Mariwata
AIBU! Msanii wa Bongo Movies, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ aliyewahi kuripotiwa kujiachia kimalovee na mwanamuziki Emmanuel Eribariki ‘Nay wa Mitego’ ametia aibu kubwa baada ya picha zake za utupu kuzagaa mitandaoni.

Pichani ni msanii wa Bongo Movies, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ katika pozi tofauti.
Kutokana na picha hizo ambazo zimeonekana kuzagaa katika mitandao mbalimbali na kuacha viulizo kwa wasanii wengi wanaomfahamu, paparazi wetu alimtafuta Bozi ambaye alionekana kutafunatafuna maneno na kumtupia lawama nzito Nay wa Mitego ambaye aliwahi kumtumia picha hizo walipokuwa wapenzi.Msanii wa Bongo Fleva Emmanuel Eribariki ‘Nay wa Mitego' akipozi na 'Bozi'.
“Mungu wangu sijui nitaweka wapi sura yangu, nilishtuka sana baada ya kuona picha hizo ni aibu kubwa kwangu, nashindwa hata kuelewa zimesambaa vipi maana hizi picha alikuwa nazo Nay, nilimtumia kabla hatujaachana sasa hata yeye namuuliza anasema eti hajazisambaza,” alisema msanii huyo huku akiomba habari hiyo isitolewe gazetini.

No comments: