Haruni Sanchawa na Makongoro Oging’KIFO cha mfanyabiashara aliyeshikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Stakishari, Ukonga jijini Dar es Salaam, Liberatus Damiani Temu (55) kilichodaiwa kilitokana na kipigo kutoka kwa askari wa kituo hicho sasa ukweli umejulikana.
Mke wa marehemu, Naomi Liberatus (katikati) akihuzunika kwa kumpoteza mwenzake.
Baada ya kusababisha ajali hiyo, ilidaiwa marehemu Liberatus
alifuatilia masuala ya bima ili aweze kumlipa aliyemgonga ambaye pia
anatajwa kuwa mteja mzuri katika Baa ya Meku iliyokuwa ikimilikiwa na
marehemu.“Watu wanasemasema tu kwamba Liberatus aliuawa na askari, si kweli. Kwa nini tumuue? Kwa kosa lipi? Sisi tulimshikilia kwa sababu hali ya majeruhi aliyemgonga ilikuwa mbaya, hivyo kumweka mahabusu marehemu ilikuwa kwa ajili ya usalama wake pia.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akifafanua jambo.
“Wengi wanaamini kila anayewekwa mahabusu ni mhalifu wa kiwango cha
kuteswa na polisi, si kweli. Wengine wanakaa hapa ili kuwalinda. Wewe
ukiua unadhani ndugu wa marehemu watakuacha?” alisema askari mmoja wa
kituo hicho bila kutaja jina lake kwa kuwa si msemaji mkuu.Alisema kuwa mahabusu waliokuwa na marehemu ni mashahidi wakubwa kwamba jamaa alijigonga kichwa ukutani lakini kabla ya kufanya hivyo, alikuwa akisemasema maneno mengi kama aliyechanganyikiwa.
Hata hivyo, marehemu amezikwa akiacha maswali kibao, watu wanajiuliza je, kilichosemwa na polisi ndiyo ukweli au la! Kufuatia utata wa kifo hicho, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ameunda tume kufuatilia sakata hilo.
No comments:
Post a Comment