welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Thursday 2 October 2014

JB: WASTARA ANAJITAMBUA

Ng’osha
BONGE la Bwana, Jacob Stephen ‘JB’ amewaasa wasanii wa kike akiwataka wajitambue ili waweze kuishi kwa muda mrefu katika gemu la sanaa.
                                          Bonge la Bwana, Jacob Stephen ‘JB’.
Akizungumza katika sherehe ya kuzaliwa msanii Wastara Juma alisema, wasanii wengi wa kike wana muda mchache sana kwenye tasnia ya sanaa, ila kwa Wastara kajitahidi sana na bado anaendelea kuishi katika sanaa kutokana na kujitambua kwake.                                Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Wastara Juma.
“Nawasihi wasanii wengine wa kike kuiga maisha ya Wastara pamoja na misukosuko ya maisha ya hapa na pale lakini bado anajitambua, anapigana na kusimama, ujue wanawake muda wao ni mchache katika sanaa tofauti na wanaume lakini kwa Wastara bado yuko,Happy birthday Wastara,’ alisema JB.

No comments: