welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Monday 1 December 2014

WANAWAKE WASUTANA KISA KUIBIANA BWANA


Wakina mama, Tabu Mohamed na Mwajuma Chota  ( katikati ) wakisutana kwa kuibiana mabwana.
Stori: Dustan Shekidele, Morogoro
Makubwa! Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikiwa kwenye msukosuko wa fedha zilizochotwa ‘kihuni’ kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, mwanaume mmoja, mtumishi wa wizara hiyo mkoani hapa almaarufu Kigogo wa Escrow, amesababisha wanawake wawili kusutana kwa matarumbeta na kukabana wakidaiwa kumgombea kwani ana fedha ‘chafu’.Tukio hilo la aina yake lilijiri wikiendi iliyopita katika Mtaa wa Karume mjini hapa ambapo wanawake hao, Tabu Mohamed na Mwajuma Chota walisababisha pakachimbika hadi polisi walipofika na kuokoa jahazi.
Awali ilifahamika kwamba wanawake hao walikuwa wakiishi pamoja maeneo ya Kikundi, Kata ya Sultan Area mkoani hapa. Kwa mujibu wa madai ya mashuhuda waliokuwa wamefunga mtaa huo, Tabu ndiye aliyeanza ‘kuchepuka’ na kigogo huyo ambaye ni mume wa mtu aliyemnunulia gari aina ya Toyota Opa.
Madai yaliendelea kushushwa kwamba, Mwajuma ambaye ni mke wa mtu alipoona mwenzake anakula vinono, naye akajiweka.

  Bendi ilikodiwa na Tabu Mohamed ili kumsuta shosti yakeMwajuma Chota.
Habari za mtaani zilidai kuwa katika kujiweka, alifanikiwa kulamba mshiko wa shilingi elfu 80 kabla ya kushtukiwa na Tabu huku naye akitaka kuhongwa gari kama mwenzake.
Ilielezwa kwamba katika kufuatilia, Tabu aligundua kuwa Mwajuma anachepuka na ‘mshefa’ wake ndipo akapanga mashambulizi ya vita vya ardhini.

Kwa hasira, Tabu alishonesha sare za ‘madila’ na kununua mizinga ya pombe kali ambapo alienda kukodi matarumbeta na watu wa kusuta.
Wakubwa kwa watoto wakishuhudia vimbwanga vya wakinamama hao. 
Ilisemekana kwamba kabla ya tukio, watu walipiga pombe kisha wakamfuata nyumbani kwao, Mtaa wa Karume na kulianzisha.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda ambalo liliwasili eneo la tukio ndani ya dakika sifuri juu ya tukio hilo, Mwajuma alifunguka: “Namshangaa Tabu kuja kunifanyia vurugu wakati na yeye ni mwizi tu. Huyo bwana ni mume wa mtu.”
Kwa upande wake, Tabu alidai Mwajuma ni shosti yake lakini alimtendea kitendo kibaya cha kutembea na bwana’ke.

Mmoja wa wamama hao, Tabu Mohamed  akichukuliwa na polisi kwa kumletea fujo mwenzake, Mwajuma Chota.
Alipobanwa zaidi hasa suala la kukodisha matarumbeta na kwamba mwanaume huyo ni mume wa mtu, Tabu alidai kwamba jamaa huyo alimkataza kuzungumza na wanahabari.
Baada ya kuipata ishu hiyo, gazeti hili liliwasiliana na mke wa kigogo huyo na kumuuliza kama ana habari kwamba kuna wanawake wanamgombea mumewe ndipo akapatwa na mshtuko na kuahidi kulifanyia kazi na kama ni kweli atafungasha virago.

Makamanda wa Polisi wakiimarisha ulinzi eneo la tukio.
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Karume, Elly Mgota alithibitisha vurugu hizo kutokea kwenye mtaa wake ambapo sakata hilo lilitinga polisi baada ya Tabu kutiwa mbaroni kwa kosa la kumfanyia fujo mwenzake.

No comments: