welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Thursday 9 October 2014

RAIS KENYATTA APOKEWA KWA SHANGWE NAIROBI


Makundi ya watu wanaoshangilia, yamempokea Rais Uhuru Kenyatta ambaye amerejea Kenya baada ya kuhudhuria Mahakama ya Kimataifa ICC, iliyopo The Hague.
Bwana Kenyatta alihudhuria shauri mahakamani siku ya Jumatano, na kuwa rais wa kwanza aliyepo madarakani kufika katika mahakama ya ICC.
Anakanusha mashtaka dhidi yake ya uhalifu dhidi ya ubinaadam kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007, zilizosababisha vifo vya watu 1,200 na wengine 600,000 kupoteza makazi.
Rais Kenyatta alipokelewa Nairobi kwa gwaride la heshima na ngoma.
Picha: Bw Kenyatta akiwa na mmoja wa mawakili wake wa utetezi ICC.

No comments: