welcome

you are welcome dj zombie blog, dodoma tanzania. for latest videos, audios and news.

Wednesday 8 October 2014

RAIS JK KUPEWA ‘KATIBA MPYA’ LEO


Rais Jakaya Kikwete,
RAIS Jakaya Kikwete, leo atapokea ‘Katiba Mpya’ inayopendekezwa kutoka kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum, Samuel Sitta, katika tukio linalotarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Bunge hilo maalum, lilihitimisha kazi yake ngumu ya kujadili rasimu ya katiba mpya iliyowasilishwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba Oktoba 4 mwaka huu, baada ya Kamati ya Uandishi chini ya Andrew Chenge kuwa imewasilisha katiba inayopendekezwa iliyokubaliwa na wajumbe kutoka Bara na Visiwani.


Katiba hiyo inayopendekezwa, ilipatikana licha ya baadhi ya wajumbe kutoka vyama vya upinzani kujitoa kwa madai ya kuburuzwa na wenzao wa chama tawala, kitendo kilichoibua mjadala wa kitaifa huku makundi mbalimbali yakipingana, wengine wakiwaunga mkono na wengine wakiwapinga.

No comments: